DODOMA
Walimu wa shule ya
msingi Chamwino B manispaa ya Dodoma wamezitaka mamlaka zinazohusika kufanya
ukaguzi wa kina kabla ya kutoa leseni kwa wafanyabiashara wanaoonyesha picha za
video kwenye mabanda mitaani.
Wakizungumza shuleni hapo na kituo hiki walimu hao wamesema
kuwa mabanda hayo yanayotumika kuonyesha picha hizo yamezagaa kila mahali bila
kujali athari zinazoweza kujitokeza kwa
watoto hasa wanafunzi.
Mwalimu wa shule
hiyo Grace Lisasi amesema kuwa wenye dhamana ya kutoa leseni ndiyo wanatakaiwa
kufanya uchunguzi na kubainisha nia wapi yanapo stahili kuwekwa mabanda hayo.
Aidha amesema kuwa
watu wanao onyesha video hizo hawana huruma na watoto kutokana na kuwarusu
kuingia na kutazama picha hizo hata pale wanapo kuwa kama wamevaa sare za shule
hali inayosababisha wengi wao kukosa masomo.
Kwa upande wao baadhi
ya wanafunzi shuleni hapo wamesema ni vyema mwanafunzi mwenyewe akajitambaua na
kuacha kuingia kwenye mabanda hayo, kwani wanapoteza muda mwingi wa masomo na
kuharibu mwelekeo wa maisha yao.
DAR ES
SALAAM
Baraza la
Habari Tanzania (MCT), limetoa idhini ya
kudumu kwa vyuo vitano vya uandishi wa habari nchini kutumia mitaala ya taifa
iliyothibitishwa na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).
Hatua hiyo imefikiwa baada ya MCT kwa kushirikiana na NACTE kufanya ukaguzi wa vyuo hivyo mwaka huu ili kubaini uwezo wao kutumia mitaala hiyo na vigezo muhimu, uwepo wa vifaa, mazingira ya taaluma, miundombinu na uongozi.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Kaimu Katibu Mtendaji wa Baraza hilo, John Mireny, amevitaja vyuo hivyo kuwa ni Dar es Salaam School of Journalism, Time School of Journalism na Royal School of Journalism vilivyoko Dar es Salaam. Vingine ni Muslim University cha Morogoro na Teofilo Kisanji cha Mbeya.
Bwana Mireny amesema kuwa vyuo hivyo vinaongeza idadi na kuwa na vyuo saba vilivyopewa idhini ya kudumu kutumia mitaala hiyo, na vingine viwili vilivyokaguliwa mwaka jana ambavyo Institute of Professional Studies kilichopo Dar es Salaam na Arusha Journalism Training College cha jijini Arusha.
Ameongeza kuwa vyuo hivyo vitakuwa vinatoa elimu kuanzia cheti hadi diploma huku vyuo vingine vitatu vikiwa tayari vimeruhusiwa kutumia mitaala hiyo kwa muda.
Amevitaja vyuo hivyo kuwa ni Kyela Polytechnic College cha Mbeya, Insitute of Social Media Studies kilichopo Arusha na Morogoro School of Journalism cha Morogoro.
Ameongeza kuwa baraza litafanya mapitio madogo ya mitaala hiyo kuanzia leo ili kufanya maboresho katika maeneo kadhaa na zoezi hilo litawahusisha walimu kutoka vyuo vya habari na wahariri waandamizi 12.
ARUSHA
Waziri mkuu mizengo pinda amewataka watendaji
mbalimbali wa ngazi ya mkoa na wilaya kuhakikisha kuwa wanakuwa na usimamizi wa
karibu ili kuhifadhi miundi mbinu ya barabara ambayo imekuwa ikitumia fedha
nyingi za serilali kwa ajili ya utengenezwaji.
Waziri mkuu Ameyaseama hayo wakati akifungua mkutano
wa wadau wa barabara za halmashauri uliofanyika Jijini Arusha wenye lengo la kutathimini
matatizo mbalimbali yanayokabili miundo mbinu ikiwemo ya barabara za halmashauri
nchini.
Kwa upande
wao wadau wa mfuko wa barabara akiwemo
waziri wa TAMISEMI Mheshiwa Hawa Ghasia amesema kuwa zipo changamoto
zinazokabili utekelezaji wa barabara huku wakitaka uanzishwajiwa wa wakala wa
usimamizi wa barabara utakaokuwa chini ya halimashauri.
Wamesema kuwa endapo miundo mbinu ya barabara hasa
za vijijini haitarekebishwa itakuwa ni vigumu kukuza uchumi wa wananchi na
taifa kwa ujumla.
Hata hivyo wajumbe kutoka halimashauri ya wilaya ya
Arusha wamesema kuwa katika mwaka wa fedha uliopita waliweza kutenga fedha
katika mapato ya ndani na kununua mitambo mbalimbali ambavyo vilifanikisha
kufanya uboreshaji wa barabara hali iliyopelekea kuwa halmashauri ya kwanza
nchini kutokana na ununuzi wa vifaa
hivyo.
DODOMA
Wafanyabiashara wa
soko kuu la majengo manispa ya Dodoma
wameiomba serikali kufungua masoko ya nje ili kuyanusuru mazao ambayo yameshuka
bei kwa kiasi kikubwa.
Mmoja wa
wafanyabiashara hao Bwana Said Kimolo ameiambia Rasi FM kuwa soko la mazao limeshuka kwa kiasi kikubwa kutokana na
masoko ya nje kufungwa.
Mfanyabiashara huyo
amesema mpaka sasa hawaelewi mpango wa serikali nini kuhusiana na soko la nje
kuwasaidia ili wapate soko la kuyapeleka mazao yaliyojaa sokoni hapo.
Amesema mji wa
Dodoma uko chini sana kibiashara hivyo serikali badala ya kukaza kuendelea
kukusanya kodi ni vizuri pia wakaangalia namna ya kuwasaidia kufungua soko la
nje ili waweze kuuza mazao waliyonayo.
Aidha amesema kuwa kingine kinachochangia upungufu wa mauzo
sokoni hapo ni vyuo vikuu vilivyopo mkoani hapa kufungwa kwa wakati mmoja tena
kwa muda mrefu wa miezi mitatu.
DAR ES
SALAAM
Serikali
imesema kuwa haipo tayari kufunga mipaka yake kwa sasa kuzuia wananchi wa nchi
zinazo kabiliwa na ugonjwa wa ebola kuingia nchini.
Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dokta Seif Rashidi, wakati akizungumza na waandishi wa habari.
Kwa sasa
ugonjwa wa ebola umezitikisa nchi kadhaa za Afrika Magharibi huku ikiripotiwa kuwa
takribani watu zaidi ya 400 nchini Liberia wamefariki Dunia huku watu
zaidi ya 1,000 wamepoteza maisha.
Waziri Rashidi amesema ili kufikia hatua hiyo ya kufunga mipaka ni lazima kuwa na makubaliano katika kanda husika na ushauri kutoka Shirika la Afya Duniani juu ya hatari inayoweza kutokea kwa nchi husika.
Wakati huo Shirika la Ndege la Kenya limesitisha safari za ndege la shirika hilo kuelekea mataifa matatu yaliyoathirika kwa kiasi kikubwa na mlipuko wa ugonjwa wa ebola.
Kenya imesema
kuwa baada ya kupata ushauri wa WHO na Wizara ya Afya ya nchini Kenya, shirika hilo limeamua
kusimamisha safari zote za ndege kwenda Liberia na Sierra Leone.
CAIRO
Kiongozi
wa ujumbe wa Wapalestina katika majadiliano ya amani
na Israel amesema kuwa ghasia zinaweza kuzuka
tena katka Ukanda wa Gaza, iwapo hakuna hatua zinazopigwa
kuelekea makubaliano ya kudumu.
Wajumbe
wa majadiliano wa Israel na Palestina
wamerefusha usitishaji mapigano, kwa lengo la
kuendeleza mazungumzo ya kumaliza mashambulizi dhidi ya
Ukanda wa Gaza.
Hata
hivyo kiongozi wa ujumbe wa Palestina Azzam al-Ahmad,
amewaambia waandishi habari mjini Cairo kuwa
hakuna hatua zilizopigwa kuhusu kipengele chochote
katika mazungumzo hayo, na kwamba ghasia huenda
zikazuka tena kabla ya muda mpya uliowekwa
wa kusitisha mapigano kumalizika.
JOHANNESBURG
Watu 9
wamefariki Dunia baada ya kuangukiwa na nyumba katika eneo la Alberton mjini Johannesburg.
Msemaji wa
shirika la huduma ya kwanza Bwana William Ntladi amesema Idadi hiyo huenda ikaongezeka
kwa kuwa baadhi ya watu bado wamekwama kwenye kifusi cha nyumba hiyo.
Timu ya
uokoaji inaendelea kufanya juhudi kuwatafuta walionusurika. Hadi sasa chanzo za
kuporomoka kwa jengo hilo bado hakijajulikana.
KIEV
Msemaji
wa wizara ya mambo ya kigeni ya Ukraine amesema kuwa Kansela
Angela Merkel wa Ujerumani atasafiri kwenda mjini
Kiev siku ya Jumamosi kwa mazungumzo ya
kisiasa kuhusu mzozo wa Ukraine.
Ziara
hiyo itafanyika katika mkesha wa sherehe za
uhuru wa Ukraine.
Wakati
huo miili ya watu 15 imepatikana hadi sasa kutoka
eneo lililoshambuliwa kwa roketi Agost 18 mwaka huu dhidi ya msafara wa mabasi
na magari madogo ya wakimbizi mashariki mwa
Ukraine.
Shambulio
hilo lilitokea karibu na mji wa Luhansk,
karibu na mpaka wa Urusi katika eneo ambalo
kumekuwa na mapigano makali kati ya majeshi
ya serikali na wapiganaji wanaotaka kujitenga
wanaounga mkono Urusi.
Jeshi
la Ukraine limewalaumu wapiganaji, na wao
wamekana kuhusika na shambulio hilo.
No comments:
Post a Comment